Sunday, October 7, 2012
SIR ALEX FERGUSON AMSIFIA DE GEA NA KUENDELEZA FOMULA YAKE YA KUBADIRISHA MAKIPA KILA MECHI!
Ingawa
Sir Alex Ferguson amemsifia Kipa wake David De Gea kwa kudaka vizuri
kwenye Mechi ya UEFA CHAMPIONS LIGI hivi juzi katikati ya Wiki
walipocheza huko Romania na CFR Cluj na kushinda bao 2-1, Meneja huyo wa
Manchester United amesema ataendelea kuwabadili Makipa katika Mechi
zijazo.
De Gea, Miaka 21, aliejiunga na Man
United Msimu uliopita, aliachwa baada ya kucheza Mechi mbili za kwanza
za Ligi Kuu England Msimu huu na namba yake kupewa Anders Lindegaard,
Miaka 28, kwenye Mechi 4 za Ligi ingawa De Gea alirudi tena na kucheza
Mechi ya UEFA CHAMPIONZ LIGI na CAPITAL ONE CUP dhidi ya Newcastle.
Mechi ijayo ya Man United ni ile ya Ligi
Jumapili huko Sport Direct Arena ambapo wataivaa Newcastle na ni juu ya
Ferguson kuamua amchezeshe Kipa toka Spain De Gea au Lindegaard kutoka
Denmark.
Kuhusu hilo, Ferguson ametamka: “Yeye De
Gea alicheza vyema na Cluj, ni Kipa mzuri sana, bado Kijana na anazidi
kuimarika. Sijajua kama nitamchezesha yeye au la lakini tulichokuwa
tukifanya katika Wiki chache zilizopita kimeenda vyema.”
Aliongeza: “Kila Mtu anataka kucheza na
Makipa sio tofauti. Lakini ninachotizama sasa ni kuwapa uzoefu wote kitu
ambacho kitatusaidia katika malengo ya muda mrefu. Ni wazi utafika
wakati mmoja wao ndio atakuwa Namba wani akionyesha uimara mfululizo na
akikomaa. Kwa sasa wote bado hawana uzoefu wa Mechi kubwa kabisa. Na
hilo watalipata baada ya muda!”

Akizungumzia Makipa kucheza wakiwa na
umri mkubwa, Ferguson alimtaja Kipa wake Edwin van der Sar aliestaafu
Mwaka 2011 akiwa na Miaka 40 na akaongeza: “Peter Schmeichel alikuwa na
Miaka 27 alipojiunga nasi na kila Mtu alimzungumzia kuwa ni Kijana
wakati alikuwa na Miaka 27 lakini alitupa Miaka 8 ya uchezaji bora.
Makipa wanaweza kucheza hata wakiwa na umri mkubwa sana wa kukaribia
Miaka 40. Mtazame Brad Friedel, na Peter Shilton kwenye Fainali za Kombe
la Dunia Mwaka 1990, alikuwa na Miaka 40!”
MOURINHO: NINA FURAHA TELE REAL MADRID ... SIONDOKI HADI NIMALIZE MKATABA MWINGINE NILIOSAINI WA MIAKA MINNE ... BAADA YA HAPO NAWEZA KURUDI ENGLAND..!
Mourinho
Mzee wa Mataji... Mourinho
MADRID, Hispania
Kocha wa Real Madrid, Jose Mourinho amesema kuwa ana furaha tele katika klabu yake inayoshikilia ubingwa wa La Liga, Ligi Kuu ya Hispania na kwamba hafikirii kuondoka kabla ya kumalizia mkataba mwingine mpya aliosaini hivi karibuni wa kubaki klabuni hapo kwa miaka minne zaidi.
Mourinho ametoa ufafanuzi huo kufuatia uvumi uliotanda kwamba yuko mbioni kurudi kufundisha katika klabu za Ligi Kuu ya England.
“Nina furaha na ninataka kubaki hapa. Nimesaini mkataba mwingine na Real Madrid utakaonibakiza kwa miaka mingine minne, ni kwa sababu sisi ni klabu bora zaidi duniani.
“Kufuatia mataji niliyotwaa England na Italia, Real Madrid ilikuwa inakosekana katika CV yangu. Na sasa kwa sababu tayari ninayo, ninapaswa kufanya kazi kwa uwezo wangu wote.
“Hata hivyo nilikuwa na furaha sana jijini London, na nitarudi tu.”
XAVI: NITAFURAHI SANA NIKIPIGA HAT-TRICK DHIDI YA REAL

Xavi
BARCELONA, Hispania
Kiungo nyota wa Barcelona, Xavi amesema kwamba kufunga mabao matatu (hat-trick) katika mechi yao ya kesho Jumapili dhid ya mahasimu wao wa jadi, Real Madrid itakuwa ni furaha ya aina yake kwani ni ndoto itakayogeuka kuwa kweli
Nyota huyo mwenye miaka 32 ameshatwaa mataji kadhaa katika ngazi zote za klabu na timu ya taifa, lakini bado anasubiri kufunga hat-trick yake ya kwanza masihani, na anaona kuwa mechi ya kesho ya 'el clasico' itakuwa ni ndoto ya kweli pindi ikitokea akafunga kweli mabao matatu peke yake.
"Kuna kitu kingine ambacho bado sijafanya? Ni kufunga hat trick... nitafurahi sana nikipiga hat-trick yangu ya kwanza dhidi ya Real Madrid," Xavi amesema huku akitabasamu kwenye mkutano na waandishi wa habari.
"Kwakweli hatudhani kwamba ushindi dhjidi yao utazidi kuongeza migogoro ndani ya kikosi cha Real Madrid. Tumedhamiria kupata ushindi, jambo ambalo litatuongezea morari kikosini."
Kiungo huyo mchezeshaji ameendelea pia kuzungumzia hali ya majeruhi kikosini mwao kama Gerard Pique, Carles Puyol na Eric Abidal, ambaye afya yake inaendelea kuimarika baada ya kufanyiwa upasuaji wa kupandikiziwa ini mwanzoni mwa mwaka huu.
"Hivi sasa, kuna nafasi ya asilimia 50 kwamba Pique atacheza dhidi ya Madrid," Xavi amesema.
"Jeraha la Puyol linasikitisha sana... yeye ni mfano ndani na nje ya uwanja kwa kila mchezaji na mara zote hucheza kwa nguvu zake zote.
"Abidal? Amehamasika sana kurejea kikosini."
Hivi sasa Barcelona wako klatika mazungumzo na wakala wa Xavi kuhusiana na mkataba wake mpya, na mchezaji huyo wa kimataifa wa Hispania anaamini kwamba makubaliano yao yanasubiri muda tu.
"Nipo katika klabu bora zaidi duniani, ningependa kustaafu nikiwa hapa. Wakala wangu anazungumza na klabu kuhusiana na mkataba mwingine mpya, hakutakuwa na tatizo lolote," amesema Xavi.
ARSENAL YANG'ARA UGENINI NA KUSHINDA 3-1 DHIDI YA WEST HAM UNITED... CHELSEA YAIUA NORWICH CITY 4-1, MAN CITY YAIKANDAMIZA SUNDERLAND 3-0, WEST BROM 3 2 QPR
Sasa nd'o nimeanza safari ya kufunga mabao kama mvua ... Olivier Giroud wa Arsenal (katikati) akifunga dhidi ya West Ham wakati wa mechi yao ya Ligi Kuu ya England kwenye Uwanja wa Upton Park leo, Oktoba 6, 2012. (Picha: BBC)
Gooooh...! Fernando Torres akiifungia Chelsea bao la kusawazisha dhidi ya Norwich.
Nahodha Holt wa Norwich akishangilia baada ya kuifungia timu yake goli la kuongoza dhidi ya Chelsea wakati wa mechi yao ya Ligi Kuu ya England leo Oktoba 6, 2012.
Safiiii... Torres wa Chelsea akipongezwa na wachezaji wenzake Juan Mata na Ivanovic baada ya kufunga goli lao la kusawazisha dhidi ya Norwich City leo.
Hazard wa Chelsea akifunga dhidi ya Norwich katika mechi yao ya Ligi Kuu ya England leo.
Thomas Vermaelen wa Arsenal (kushoto) akichuana na Andy Carroll wa West Ham wakati wa mechi yao ya Ligi Kuu ya England leo Oktoba 6, 2012.
LONDON, England
Olivier Giroud alifunga goli lake la kwanza la Ligi Kuu ya England akiwa na Arsenal wakati 'Gunners' wakicharuka kutoka kuwa nyuma na kushinda ugenini kwa mabao 3-1 dhidi ya West Ham jkwenye Uwanja wa Boleyn Ground, Upton Park jijini London usiku huu.
West Ham walipata goli la utangulizi kinyume na mwelekeo wa mechi katika dakika ya 21 wakati mshambuliaji wa kimataifa wa Sengal, Mohamed Diame alipopiga shuti kali la 'upinde' lililomshinda kipa Vito Mannone na kujaa wavuni.
Giroud alisawazisha kabla ya mapumziko wakati alipoiwahi krosi ya Lukas Podolski na kuiunganishia wavuni, pembeni kwa ndani ya mlingoti wa goli.
Kevin Nolan alikosa nafasi mbili za wazi kuwapa wenyeji uongozi na aliadhibiwa baada ya Santi Cazorla kuifungia Arsenal bao la pili na mtokea benchi Theo Walcott aliyechukua nafasi ya Gervinho akaongeza goli la tatu wakati Arsenal wakicheza gonga safi huku West Ham wakionekana 'kutepeta'.
Giroud alifunga goli lake la kwanza katika ligi kuu ya England tangu atue Arsenal akitokea Ufaransa mwanzoni mwa msimu huu na kucheza kwa dakika 303 bila mafanikio. Goli hilo lilitokana na shuti lake la 12 (jumla 15, ukichanyanya na yaliyoyozuiwa) tangu aanze kucheza katika ligi kuu ya England.
Katika mechi nyingine zilizochezwa leo, Man City iliikandamiza Sunderland kwa mabao 3 - 0, Chelsea ikashinda 4-1 dhidi ya Norwich, Swansea na Reading zikatoka sare ya 2 - 2, West Brom wakazidi kuiweka pabaya Queen's Park Rangers kwa kuichapa mabao 3 - 2 na Wigan na Everton pia zikatoka sare ya 2 - 2.
HAPPY BIRTHDAY MHESHIMIWA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE!!!
Tarehe ya leo Oktoba 7 ni siku aliyozaliwa Rais wetu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Mrisho kikwete(JK). BUKOBASPORTS.COM
inaungana na maelfu ya wananchi wa Tanzania na Duniani nzima
waliomtakia maisha mema na wanaoendelea kumpongeza kwa siku hii. Sisi
Bukobasports tunamtakia maisha marefu na ya afya njema na Mungu amjalie
ili aweze kuliongoza Taifa letu vema.
Mc DONALD MARIGA AFUKUZIWA NA FULHAM, READING..!

MacDonald Mariga.
![]() |
| MacDonald Mariga wa Inter Milan akishangilia baada ya kufunga goli la tatu dhidi ya Genoa kuwania Kombe la Tim kwenye Uwanja wa Giuseppe Meazza mjini Milan, Januari 12, 2011. |
Kiungo wa klabu ya Inter Milan inayoshiriki Serie A, Ligi Kuu ya Italia, Mkenya McDonald Mariga anafukuziwa na klabu kadhaa za Ligi Kuu ya England zikiwamo za Fulham na Reading, imefahamika.
McDonald akifanya mazoeziGazeti la Tuttosport limesema leo kuwa Fulham na Reading zinajiandaa kumfukuzia kiungo huyo wa timu ya taifa ya Kenya 'Harambee Stars' wakati wa dirisha dogo la usajili wa Januari.
Inadaiwa kuwa Inter imepokea ofa kadhaa za kumsajili kiungo huyo mwenye miaka 25, zikiwamo za Fulham na Reading.
KUHUSU Mc DONALD
Born: April 4, 1987 (age 25), Nairobi
Height: 1.88 m
Weight: 86 kg
Salary: $700,000 EUR (2012)
Siblings: Victor Wanyama, Thomas Wanyama, Sylvester Wanyama, Mercy Wanyama
Parents: Noah Wanyama, Mildred Wanyama
MBWANA SAMATTA, TRESSOR MPUTU WATOSWA KATIKA ORODHA YA NYOTA 34 WANAOWANIA TUZO YA MWANASOKA BORA WA AFRIKA 2012... WAMEJAA 'MAPROO' WA ULAYA KAMA YAYA TOURE, DEMBA BA, GERVINHO, PAPISS DEMBA CISSE ... WANAOCHEZA AFRIKA NI WATATU TU AMBAO NI MSAKNI WA ESPERANCE YA TUNISIA, RAINFORD KIDIABA NA STOPHILA SUNZU WA TP MAZEMBE YA DR CONGO
Mbwana Samatta
Tressor Mputu
Yaya Toure
CAIRO, Misri
Shirikisho la Soka la Afrika (CAF) limetaja majina ya awali ya wachezaji nyota 34 barani wanaowania tuzo ya Mwanasoka Bora wa Afrika Mwaka 2012 ambamo ndani yake, wamejaa 'maproo' 29 wanaocheza soka la kulipwa nje ya Afrika huku nyota wa TP Mazembe, Mtanzania Mbwana Samatta na Tressor Mputu wanaong'ara katika Ligi ya Klabu Bingwa Afrika wakikosekana kwenye orodha hiyo.
Miongoni mwa wanaocheza soka la kulipwa Ulaya ni mshindi wa tuzo hiyo msimu uliopita, kiungo wa timu ya taifa ya Ivory Coast na klabu ya Manchester City ya England, Yaya Toure, mastraika nyota wa Newcastle United -- Papiss Demba Cisse na Demba Ba na pia winga wa Arsenal, Gervinho..
Wachezaji watatu wanaocheza katika klabu za Afrika ni Wazambia Rainford Kalaba na Stoppila Sunzu wanaoichezea TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Youssef Msakni wa Esperance ya Tunisia.
Orodha kamili:
1. Abdelaziz Barrada - Getafe (Hispania) na Morocco
2. Adel Taarabt - Queens Park Rangers (England) na Morocco
3. Alain Sibiri Traore - Lorient (Ufaransa) na Burkina Faso
4. Alexander Song - Barcelona (Hispania) na Cameroon
5. Andre 'Dede' Ayew - Marseille (Ufaransa) na Ghana
6. Arouna Kone - Wigan (England) na Ivory Coast
7. Aymen Abdennour - Toulouse (Ufaransa) na Tunisia
8. Bakaye Traore - AC Milan (Italia) na Mali
9. Cheick Tiote - Newcastle United (England) na Ivory Coast
10. Christopher Katongo - Henan Construction (China) na Zambia
11. Demba Ba - Newcastle United (England) na Senegal
12. Didier Drogba - Shanghai Shenhua (China) na Ivory Coast
13. Emmanuel Agyemang-Badu - Udinese (Italia) na Ghana
14. Emmanuel Mayuka - Southampton (England) na Zambia
15. Foxi Kethevoama - FC Astana (Kazakhstan) na Afrika ya Kati.
16. Gervinho - Arsenal (England) na Ivory Coast
17. Hilaire Momi - Le Mans (Ufaransa) na Afrika ya Kati.
18. John Obi Mikel - Chelsea (England) na Nigeria
19. John Utaka - Montpellier (Ufaransa) na Nigeria
20. Kwadwo Asamoah - Juventus (Italia) na Ghana
21. Moussa Sow - Fenerbahce (Uturuki) na Senegal
22. Nicolas N'koulou - Marseille (Ufaransa) na Cameroon
23. Papiss Demba Cisse - Newcastle United (England) na Senegal
24. Pape Moussa Konate - FC Krasnodar (Urusi) na Senegal
25. Pierre-Emerick Aubameyang - St Etienne (Ufaransa) na Gabon
26. Rainford Kalaba - TP Mazembe (DR Congo) na Zambia
27. Seydou Doumbia - CSKA Moscow (Urusi) na Ivory Coast
28. Seydou Keita - Dalian Aerbin (China) na Mali
29. Sofiane Feghouli - Valencia (Hispania) na Algeria
30. Stoppila Sunzu - TP Mazembe (DR Congo) na Zambia
31. Victor Moses - Chelsea (England) na Nigeria
32. Yaya Toure - Manchester City (England) na Ivory Coast
33. Younes Belhanda - Montpellier (Ufaransa) na Morocco
34. Youssef Msakni - Esperance (Tunisia) na Tunisia
Wakiwa kwao uwanja wa Etihad leo Timu ya
Manchester City imefanikiwa kuifunga timu ya Sunderland na kujikuta
wanapata pointi 15 nyuma ya timu ya Chelsea yenye pointi 16.Mabao ya Aleksandar Kolarov, Sergio Aguero na James Milner yameipa Manchester City ushindi wa 3-0 katika Ligi Kuu ya England joni hii dhidi ya Sunderland. Ushindi huo, umeifanya Man City itimize pointi 15 baada ya kucheza mechi saba na inashika nafasi ya pili, nyuma ya Chelsea inayoongoza kwa pointi zake 16, ambayo hivi sasa inacheza mechi ya saba nayo dhidi ya Norwich. Na mpaka sasa chelsea inaongoza goli 2 dhidi ya Norwich ikiwa na goli 1 na ni dk ya 24 mpaka sasa, chelsea wakishinda watakuwa na pointi 19.
Kolarov akipongezwa kufunga bao la kwanza Uwanja wa Etihad
Mserbia huyo anafunga bao la kuongoza kwa mpira wa adhabu
Aguero anagunga la pili 2-0 kipindi cha pili

Lilikuwa shuti la pili la Aguero tangu aingie na anafunga
Mabingwa hao watetezi sasa wapo jirani na Chelsea kileleni mwa Ligi Kuu

Balotelli akiumaliza Uwanja baada ya kutolewa
VIKOSI:
Sunderland: Gordon, Bardsley,
Nosworthy, Collins, Chimbonda, Malbranque, Leadbitter (Murphy 60), Reid,
Richardson, Cisse (Stokes 60), Diouf (Healy 60).
Subs Not Used: Ward, Miller, Yorke, Higginbotham.
Booked: Bardsley, Healy, Richardson, Chimbonda.
Man City: Hart, Corluka, Richards (Ben-Haim 46), Dunne, Michael Ball, Ireland, Hamann, Johnson (Gelson 81), Kompany, Wright-Phillips (Elano 85), Jo.
Subs Not Used: Schmeichel, Garrido, Evans, Sturridge.
Booked: Richards, Kompany.
Goals: Ireland 45, Wright-Phillips 50, 58.
Att: 39,622
Ref: Chris Foy (Merseysid
Subs Not Used: Ward, Miller, Yorke, Higginbotham.
Booked: Bardsley, Healy, Richardson, Chimbonda.
Man City: Hart, Corluka, Richards (Ben-Haim 46), Dunne, Michael Ball, Ireland, Hamann, Johnson (Gelson 81), Kompany, Wright-Phillips (Elano 85), Jo.
Subs Not Used: Schmeichel, Garrido, Evans, Sturridge.
Booked: Richards, Kompany.
Goals: Ireland 45, Wright-Phillips 50, 58.
Att: 39,622
Ref: Chris Foy (Merseysid
HABARI KUTOKA TFF
>
LIGI DARAJA LA KWANZA KUANZA OKTOBA 20
Kamati
ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ilikutana jana
(Oktoba 5 mwaka huu) kupitia na kufanya uamuzi katika masuala mbalimbali
na kupanga Ligi Daraja la Kwanza (FDL) ianze kutimua vumbi Oktoba 20
mwaka huu.
Timu zimepangwa katika makundi matatu ya
timu nane nane ambapo zitacheza ligi hiyo kwa mtindo wa nyumbani na
ugenini. Mshindi wa kila kundi ndiye atakayepata tiketi ya kucheza Ligi
Kuu ya Vodacom (VPL) msimu ujao wakati timu ya mwisho kila kundi
itashuka daraja kurudi Ligi ya Mkoa.
Kundi A lina timu za Burkina Moro ya
Morogoro, Kurugenzi Mufindi ya Iringa, Majimaji ya Songea, Mbeya City ya
Mbeya, Mlale JKT ya Ruvuma, Mkamba Rangers ya Morogoro, Polisi Iringa
na Small Kids ya Rukwa.
Ndanda FC ya Mtwara, Ashanti United,
Green Warriors, Moro United, Polisi, Tessema, Transit Camp na Villa
Squad zote za Dar es Salaam ndizo zinazounda kundi B wakati kundi C ni
Kanembwa JKT ya Kigoma, Morani ya Manyara, Mwadui ya Shinyanga, Pamba ya
Mwanza Polisi Dodoma, Polisi Mara, Polisi Tabora na Rhino Rangers ya
Tabora.
Ada ya ushiriki wa ligi ni sh. 200,000
zinazotakiwa kulipwa kabla ya Oktoba 13 mwaka huu. Pia Oktoba 13 mwaka
huu kutakuwa na kikao kati ya wenyeviti wa klabu zote zinazoshiriki ligi
hiyo na Kamati ya Ligi ambapo pia itafanyika draw (ratiba).
MECHI YA KAGERA SUGAR, YANGA YASOGEZWA
Kamati ya Ligi imesogeza mbele kwa siku
moja mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Kagera Sugar na Yanga
iliyokuwa ichezwe kesho (Oktoba 7 mwaka huu) mjini Bukoba kutokana na
Uwanja wa Kaitaba kuwa na shughuli nyingine za kijamii.
Sasa mechi hiyo itachezwa Jumatatu
(Oktoba 8 mwaka huu) kwenye uwanja huo huo. Mabadiliko hayo pia
yameathiri mechi kati ya Toto Africans na Yanga iliyokuwa ichezwe Oktoba
10 mwaka huu Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza. Mechi hiyo sasa
itachezwa Oktoba 11 mwaka huu.
WAAMUZI WATATU WAONDOLEWA, SIMBA YAPIGWA FAINI
Kamati ya Ligi imewaondoa waamuzi watatu
wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kwa kushindwa kumudu michezo
waliyopangiwa. Waamuzi hao ni Mathew Akrama wa Mwanza aliyechezesha
mechi namba 80 ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Yanga na Simba
iliyochezwa Oktoba 3 mwaka huu.
Wengine ni Paul Soleji wa Mwanza
aliyechezesha mechi kati ya Simba na Tanzania Prisons, na mwamuzi
msaidizi namba mbili kwenye mechi hiyo Mwarabu Mumbi wa Morogoro. Pia
mwamuzi msaidizi namba mbili wa mechi ya Yanga na Simba, Ephrony Ndissa
wa Dar es Salaam amepewa onyo.
Kamishna wa mechi namba 28 kati ya Yanga
na African Lyon, Pius Mashera ameondolewa kwenye orodha ya makamishna
wa ligi hiyo kwa kuchelewa kufika kwenye kikao cha maandalizi ya mechi
(Pre match meeting) na uwanjani.
Vilevile Mashera kwenye ripoti yake
aliwasilisha malalamiko dhidi ya msimamizi wa kituo cha Dar es Salaam,
na kwa vile suala hilo ni la kinidhamu ametakiwa alipeleke kwenye Kamati
ya Nidhamu na Usuluhishi ya TFF.
Nayo Simba imepigwa faini ya jumla ya
sh. 600,000 kwa kuchelewa kufika kwenye pre match meeting ya mchezo wao
dhidi Tanzania Prisons (sh. 100,000) na kwa washabiki wake kuwatupia
chupa za maji waamuzi wa mechi hiyo (500,000).
Pia Kamati ya Ligi imeagiza kuwa kwa
vile suala la kipa Shabani Kado wa Mtibwa Sugar kudaiwa kumpiga kiongozi
mmoja wa Ruvu Shooting mara baada ya mechi kati ya timu hizo
iliyochezwa Uwanja wa Azam Complex ni la kinidhamu lipelekwe kwenye
Kamati ya Nidhamu na Usuluhishi ya TFF.
YANGA, AFRICAN LYON KUTOVAA BEJI YA MDHAMINI
Kwa vile msimu huu mdhamini mwenyewe
ndiye anayegawa vifaa kwa timu, Kamati ya Ligi imeagiza Vodacom
iandikiwe barua na nakala kwa klabu zote ili kujua timu ambazo tayari
zimekabidhiwa vifaa hivyo zikiwemo logo na siku ambapo timu husika
zilipokea.
Baada ya majibu ya Vodacom ndipo Kanuni
za Ligi Kuu zitakapotumika kutoka adhabu kwa timu ambazo zitabainika
kuwa zilipokea vifaa lakini hazikuvitumia.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
REFA ALIYECHEZESHA MECHI YA YANGA NA SIMBA AONDOLEWA LIGI KUU
Kamati ya Ligi imewaondoa waamuzi watatu wa Ligi Kuu ya
Vodacom (VPL) kwa kushindwa kumudu michezo waliyopangiwa. Waamuzi hao ni
Mathew Akrama wa Mwanza aliyechezesha mechi namba 80 ya Ligi Kuu ya
Vodacom (VPL) kati ya Yanga na Simba iliyochezwa Oktoba 3 mwaka huu. Wengine ni Paul Soleji wa Mwanza aliyechezesha mechi kati ya Simba na Tanzania Prisons, na mwamuzi msaidizi namba mbili kwenye mechi hiyo Mwarabu Mumbi wa Morogoro. Pia mwamuzi msaidizi namba mbili wa mechi ya Yanga na Simba, Ephrony Ndissa wa Dar es Salaam amepewa onyo.
Kamishna wa mechi namba 28 kati ya Yanga na African Lyon, Pius Mashera ameondolewa kwenye orodha ya makamishna wa ligi hiyo kwa kuchelewa kufika kwenye kikao cha maandalizi ya mechi (Pre match meeting) na uwanjani.
Vilevile Mashera kwenye ripoti yake aliwasilisha malalamiko dhidi ya msimamizi wa kituo cha Dar es Salaam, na kwa vile suala hilo ni la kinidhamu ametakiwa alipeleke kwenye Kamati ya Nidhamu na Usuluhishi ya TFF.
Nayo Simba imepigwa faini ya jumla ya sh. 600,000 kwa kuchelewa kufika kwenye pre match meeting ya mchezo wao dhidi Tanzania Prisons (sh. 100,000) na kwa washabiki wake kuwatupia chupa za maji waamuzi wa mechi hiyo (500,000).
Pia Kamati ya Ligi imeagiza kuwa kwa vile suala la kipa Shabani Kado wa Mtibwa Sugar kudaiwa kumpiga kiongozi mmoja wa Ruvu Shooting mara baada ya mechi kati ya timu hizo iliyochezwa Uwanja wa Azam Complex ni la kinidhamu lipelekwe kwenye Kamati ya Nidhamu na Usuluhishi ya TFF.

No comments:
Post a Comment