maporomoko

maporomoko

Friday, August 31, 2012

mkutano wa 11 WA LVRLAC ULIOWAJUMUISHA WATENDAJI ZAIDI YA 450 KUTOKA NCHI ZOTE ZINAZOUNDA AFRICA MASHARIKI.

Kama ilivyo ada KASIBANTE FM REDIO  walirusha laivu kila kitu



Zawadi kwa wadhamini wa mkutano huo nazo zilitolewa.

Pale kati nini washiriki wakisikilizia 

Mhe.Meya wa manispaa ya bukoba ANATORY AMANI akiwa katika pozi la kuchati na wenzie.


Picha ya pamoja ya washiriki wa mkutano mkuu wa 11 wa LVRLAC


Halmashauri za Miji na Wilaya zinazozunguka Ziwa Victoria, zimeshauriwa kushirikisha jamii katika mipango ya hifadhi mazingira, kwa lengo la kuifanya iwe endelevu.

Mkuu wa mkoa wa KAGERA, kanali mstaafu FABIAN MASSAWE, ametoa ushauri huo wakati akifungua Mkutano wa 11 wa Umoja wa  Halmashauri 130 kutoka UGANDA,    KENYA na TANZANIA,-   LVRLAC.

Katika hotuba yake ya ufunguzi kwa niaba ya rais JAKAYA KIKWETE, kanali MASSAWE amesisitiza ushirikishwaji na uwazi kuwa ni mambo muhimu katika utekelezaji wa mipango mbalimbali ya maendeleo.

Aidha, ameonya kuwa juhudi za pamoja zinahitajika kulinda raslimali za Ziwa Victoria, ambazo zinatoweka kwa kiwango cha kutisha kutokana na uharibifu wa mazingira.
Amesema kuwa vitendo vya uvuvi haramu na matumizi ya zana haramu vinazidi kuongezeka na kutishia uhai wa ziwa hilo.

Ameonya kuwa endapo hatua za dhati hazitachukuliwa, kuna hatari ya Ziwa hilo kutoweka katika uso wa dunia.

Takriban Washiriki  450  wakiwemo  Wakurugenzi wa Halmashauri, Mameya na Wenyeviti wa Halmashauri 28 za Tanzania wamehudhuria  Mkutano huo, ambao umefanyika  katika viwanja vya GYMKHANA, katika  Manispaa ya BUKOBA.

Wednesday, August 29, 2012

DINA PAT ILIYOWASHIRIKISHA ZAIDI YA WATENDAJI 450 KUTOKA ALIMASHAURI MBALIMBALI AMBAZO NI WANANCHAMA WA LVRLAC YANI MUUNGANO WA ALIMASHAURI 130 KUTOKA KATIKA NCHI ZA TANZANIA,BURUNDI,RWANDA,UGANDA NA KENYA.HII KITU NI NDANI YA BUKOBA CLUB MKOANI KAGERA.


Hapa wakubwa wanawasili ndani ya viwanja vya BUKOBA CLUB ambapo mpango mzima ulitake place palepale.
Huu ni mfano tu wa meza za wadau jinsi zilizvyokuwa.

Kushoto ni kanali mstaafu Fabiani Masawe baada ya kumkaribisha jembe waziri wa afrika mashariki mhe.Samweli Sita ili afungua DINNA hiyo wadau wapate kuserebleiti.
Jembe baada ya kuambiwa uwanja ni wake akaanza kutoa vitu.
mwenyekiti wa LVRLAC hapa nchini Tanzania DCT Anaotry Amani ambaye pia ni mstahiki meya wa manispaa ya bukoba akapata kuongea neno baada ya kupokea ugeni huu mkubwa.




Huyu mzee kati ni msema chochote ni noma yuko vizuri katika kila lugha.
Muda ukawadia majembe kama ilivyo ada foreni ndio mpango Sita akawa wa kwanza kama mgeni Rasimi.

umesema hizi ni BIFU au?
Haaaaaaaaa imetosha weka kidogo.

DCT Anatory katika foreni ya msosi 
Sherehe ni kula bwana asikwambie mtu sasa baada ya meza ya protocal. hapa kila aliyeudhuria akapata nafasi yakujivinjari yeye mwenyewe na sahani yake.

Ngoma ya kihaya pia ilikuwepo


THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
              press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425




PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
              P.O. BOX 9120,  
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia Salamu za Rambirambi Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, Mhashamu Baba Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa kufuatia kifo cha Askofu wa Kwanza wa Jimbo Katoliki la Mpanda, Baba Askofu William Pascal Kikoti.

Kifo cha Askofu Kikoti kilitokea jana Jumanne tarehe 28 Agosti, 2012 katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Mkoani Mwanza alikokuwa amelazwa kwa matibabu kutokana na ugonjwa wa Shinikizo la Damu.

“Nimeshtushwa, nimesikitishwa na kuhuzunishwa sana kutokana na taarifa za kifo cha Baba Askofu William Pascal Kikoti wa Jimbo Katoliki la Mpanda akiwa bado na umri mdogo wa miaka 55 wakati ndiyo kwanza utumishi wake ulikuwa ukihitajika zaidi”, amesema Rais Kikwete katika Salamu zake na kuongeza,

“Ni dhahiri kwamba kifo cha Baba Askofu Kikoti kimeacha pengo kubwa la kiuongozi siyo tu kwa Kanisa Katoliki hapa nchini, bali pia Jumuiya ya Waamini wa Kanisa hilo kote duniani”.

Rais Kikwete amesema anatambua jitihada kubwa za Marehemu Baba Askofu William Pascal Kikoti enzi za uhai wake katika kuwatumikia Waumini wa Kanisa lake, na hususan wa Jimbo Katoliki la Mpanda, tangu alipopata Daraja la Upadre mwaka 1988, kuteuliwa kwake kuwa Askofu wa Kwanza wa Jimbo Katoliki la Mpanda mwaka 2000, na hatimaye alipowekwa Wakfu na Kusimikwa kuwa Askofu wa Jimbo hilo mwaka 2001.

“Kutokana na msiba huo mkubwa, ninakutumia wewe Baba Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania Salamu zangu za Rambirambi, na kupitia kwako kwa Kanisa Katoliki na kwa Waumini wote wa Kanisa hilo hapa nchini hususan wa Jimbo Katoliki la Mpanda, kwa kumpoteza mmoja wa Viongozi muhimu na wa ngazi ya juu wa kiroho, Marehemu Baba Askofu William Pascal Kikoti”, ameongeza kusema Rais Kikwete.

Amesema anamuomba Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema aipumzishe mahala pema peponi Roho ya Marehemu.  Amewahakikishia wote waliofikwa na msiba huo kuwa yuko pamoja nao katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo kwa kutambua kuwa yote ni mapenzi yake Mola. 

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.

KUTANA NA KIKUNDI CHA KUDHIBITI KANSA NCHINI TANZANIA.


KUTANA NA DKT NYAKUBAHO .Y.NYAKUJANGA. dakitari maharufu Tanzania ambaye utibu magonjwa yote kwa kutumia miti shamba hakuna ugonjwa alio wahi kushindwa dokita huyu ila sema tu vyombo vya habari vimekaa mbali naye.

DKT NYAKUBAHO .Y.NYAKUJANGA.
AKIWA KATIKA SURA YA KAZI KATIKA MAONYESHO YA AFRIKA MASHARIKI YANAYO ENDELEA KATIKA VIWANJA VYA JIMKANA KATIKA MANISPAA YA BUKOBA MKOANI KAGERA NCHINI TANZANIA.



Kama kawaida baada ya vijana kutupia jicho katika blog hii wakaona magonjwa anayo yatibu dokita huyu wakaaanza kumfikia lakini wajua dawa nyingi inayochukuliwa na vijana wa haina hii mi sijibu mwenye wasiliana na dokita mwenyewe ueleze nini kinakusibu hata kwa ushauri tu wa dokita huyu utapona wahi bado hujachelewa 

Rais wa Senegal ataka Bunge la Senate lifutwe ili fedha itumike kuokoa maisha ,

Rais wa Senegal, Macky Sall ametoa wito wa kufutiliwa mbali kwa bunge la Senate, huku pesa ambazo hutumika kulipia shughuli za bunge hilo akiagiza zitumike kwa msaada wa chakula.

Rais huyo ametoa agizo hilo baada ya kukatiza ziara yake nchini Afrika Kusini ili kushugulikia mafuriko makubwa yaliyoikumba nchi hiyo na kusababisha vifo vya watu 13.

Akiongea katika uwanja wa ndege wa Dakar rais Macky Sall, amesema kuwa atawasilisha mwaada huo wa dharura bungeni ili kufutilia mbali bunge la Senate.

amesema kiasi cha pesa Pesa ambazo hutumiwa na bunge hilo ni takriban dola milioni 15, ambazo zitaweza kutumika kuzuia na kuwasaidia waathirika wa  mafuriko kwa siku za usoni.

Ingawa maeneo ya nyanda za chini nchini Dakar hukumbwa na mafuriko kila msimu wa mvua, mwaka huu athari zimekuwa kubwa kwa sababu ya mvua kubwa iliyonyesha katika maeneo mengi ya Afrika Magharibi ambapo Inakisiwa kuwa maelfu ya watu wameachwa bila makao.

Hapo awali, wananchi walifanya maandamano kutuhumu serikali kwa kushindwa kuchukua hatua mbadala za kukabiliana vilivyo na hali hiyo ya mafuriko ingawa walitawanywa na gesi ya kutoa machozi.

Mwezi Mei mwaka huu, Benki ya Dunia iliahidi kutoa dola milioni 55.6 ili kuweza kuimarisha miundo mbinu itakayowezesha nchi hiyo kukabiliana na mafuriko.

Nchi hiyo imekuwa mfano mzuri wa nchi yenye demokrasia barani Afrika ikiwa na mfumo mzuri wa siasa za vyama vingi na mfumo wa majimbo.

SOURCE WAVUTI..

umewahi kusikia kitegera hili kwa wanakagera ni kitu cha kawaida.mcheki bwana william rutta akiwa katika kinywaji kwa kutumia kitegera.







Katika kuendeleza utalii wa ndani, mdau William Rutta akifahamika sana kwa jina la Willy Kiroyera Tours alitembelea maeneo ya Ishozi Kabyaile na kukutana wajasiliamali wakitegeneza orubisi kutoka kwenye kifaa chake maalum kijulikanacho kwa kihaya Obwato
 
 ORUBISI_AKITEGELA.JPG
 
 
 
Kitu cha kwanza ilikuwa kuwaonyesha  kuwa Willy anaweza kutegeneza Orutegera na kunywea kwenye majani hayo ya mogomba. Je unajua majani ya migomba yanatumika kwa mara 21 kwa njia tofautI- Inafutata ( oluhompo, ekitegera, omwamvuli, endosho, eshaani yo kulilao, nyingine baadae)
 
_amalula.JPG

WE UNAYEWAPENDA SENENE WAJUA HISTORY YAO? SOMA HAPA UELIMIKE.



Kwa kutumia vyanzo mbalimbali na imekuzwa na William Rutta – Kiroyera tours www.kiroyeratours.com

KUNA aina nyingi za wadudu ambao katika baadhi ya makabila hapa nchini hutumiwa kama kitoweo,na pia katika uzalishaji wa bidhaa za vyakula kwa ajili ya matumizi mbalimbali.

Senene ambao hupatikana kwa wingi mwishoni mwa kila mwaka, ni miongoni mwa wadudu wanaotumiwa zaidi na kabila la wahaya mkoani Kagera kama kitoweo, pengine kuliko kabila jingine unalolifahamu.

Hata hivyo pamoja na kitoweo hiki kupewa heshima kubwa na hata kuwa sehemu ya mila na utamaduni wa kabila hili,asili na chanzo cha senene limeendelea kuwa swali gumu miongoni mwa wenyeji wa mkoa huu.

Wahenga walisema ‘uzee dawa’na katika kutafuta majibu ya siri ya senene katika kabila hili,safari yangu ilinikutanisha na mzee David Zimbihile(80) aliyekuwa mbunge wa kwanza wa jimbo la Ihangiro sasa ni Muleba Kusini.

Wakati wa uongozi wake alikuwa na mvuto mkubwa kwa wapiga kura,na hadi leo anakumbukwa kama kiongozi ambaye utawala wake ulikuwa na baraka za wingi wa senene kila mwaka.

Anasema katika moja ya kampeini zake aliwahi kulalamikia kukosekana kwa mboga,na badala yake aliomba senene .Sara zake zilisikika na kuanzia wakati huo wananchi wakaendelea kumwamini huku madai ya uwezo wake wa kuleta senene yakitumika kutetea nafasi yake.

Mzee Zimbihile anasema pamoja na kupata umaarufu kupitia kitoweo cha senene miongoni mwa wapiga kura,anasema hakuwa na uwezo huo na kudai aliwaomba na Mungu akasikia sara zake kutokana na uhaba mkubwa wa mboga uliokuwepo wakati huo.

Hata hivyo pamoja na kusema senene ni kitoweo kinachoheshimika bado hakuweza kufahamu asili yake na sababu za wadudu hao kuvutiwa na mazingira ya mkoa wa Kagera katika misimu miwili kwa mwaka.
Anaamini ni uwezo na mapenzi ya Mungu,huku akikumbuka wakazi wa eneo la Bunya katika nchi ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC) walivyomshanga wakati alipokuwa wanakamata na kula senene enzi hizo akifanya kazi nchini humo.

Maswali yangu hayakupata majibu na alihitimisha mazungumzo kwa kusisitiza kuwa tamaa ya kula senene iliwafanya wanaume kuwaongopea wanawake kuwa kama wangekula kitoweo hicho kingeweza kuwadhuru.
Hata nilipozungumza na Saida Sarehe(67)mkazi wa eneo la Kashai mjini hapa,alidai hakuna historia yoyote kwenye kabila lao inayoeleza chanzo na asili ya wadudu hao na kudai Mungu aliitoa kama neema kwa wakazi wa mkoa huo.

Ni muuguzi mstaafu ambaye anaishia kunisimulia jinsi wasichana wa enzi zao walivyopeleka senene kwa wachumba wao,ambaye hakufanya hivyo ilimaanisha uwezekano wa kuolewa na mchumba wake ulikuwa mdogo.Senene walitumika kama ishara ya upendo na uaminifu.Anasema hawakuruhusiwa kula senene na kudai vitisho vya wanaume vilivyojificha kwenye tamaa na uroho wa senene viliwafanya wale kitoweo hicho kwa siri kubwa.

Bila kunipa majibu ya maswali yangu,analalamikia ubabe wa wanaume uliowakataza kula vitu vitamu na kuanzia hapo ananipa siri ya eneo la mkoa huu kuitwa Buhaya. Kuna baadhi ya vitu vitamu vingine kama kuku, nyama ya mbuzi, mayai wakina mama hawakurusiwa kula. Wazee wa kihaya kimila walidai mwanamke alikuwa haruhisiwi kutmumia vile kizazi kilikua shida na kwa kutumia mayai, nyama ya mbuzi na kuku wangenenepa na kushindwa kuzaa kwa wepesi ikawa ni mwiko, Bibi yangu Felista Nyamwiza aliyafariki mwaka 2010 akiwa namika 88 hakuwahi kula senene, yai wala kuku katika maisha yake yote pamoja na kutuandalia senene sisi wajukuu zake.

Kwamba wanawake walionywa wawe na haya siku zote, na wasivunje mwiko kwa kula vitu walivyokatazwa.Wote walikuwa na utii wakiheshimu mila na desturi za kabila lao.Walifundishwa kuwa na haya wasichana wa Buhaya.

Hata Khadija Khalphan(84)mkazi wa Kashai mjini Bukoba mbali na kufahamu umuhimu na nafasi ya kitoweo cha senene katika mila za kabila lake anakiri kutofahamu chanzo na asili ya wadudu hao.Hata mvua za vuli zinazoanza mwezi Novemba ambazo huambatana na ujio wa senene ,msimu huo hutambuliwa na wenyeji kwa jina la mvua za Omusene ikiwa na maana halisi ya mvua za msimu wa senene.
Pamoja na senene kuwa ishara ya neema katika kabila hili,pia inadaiwa ni dalili za kuwepo tukio baya endapo mtu ataota kuona senene wengi.

Juhudi za kufahamu siri ya senene zinanifikisha katika kituo cha Utafiti wa Kilimo Maruku,na baada ya kushindwa kumpata mtaalamu wa sayansi ya wadudu niliamua kutafuta majibu kwenye vyanzo mbalimbali kwenye mtandao wa intaneti.

Zipo aina nyingi za senene ambapo wale ninaowazungumzia wamegawanyika katika kundi lijulikanalo kwa kitaalamu kama Orthopterous na huzaliana kwa wingi katika mwambao wa maziwa makuu,baada ya kutaga mayai yao ardhini kipindi cha kiangazi.

Baada ya kutaga mayai na kuanguliwa,mzunguko wa maisha yao huisha kati ya mwezi Octoba na Desemba ambapo huruka wakiwa katika makundi makubwa wakihitimisha safari ya maisha yao.Senene hao ambao wako katika jamii ya nzige pia hutofautiana kutegemea mazingira yaliyopo na hali ya hewa, na tangu zamani hupenda kuweka makazi yao juu ya vilima.

Kwa mujibu wa vyanzo vya mtandao katika nchi ya Japan senene wa kijani humaanisha dalili njema,na mwanzo mzuri wenye matumaini ambapo pia hutumika katika utengenezaji wa chokoleti.
Hii ni aina ya panzi wapole ambao hawana tabia ya kuharibu mazao na kuteketeza makazi yao kwa chakula kama walivyo jamii ya nzige.

Hawa ni aina ya panzi ambao baada ya kuzaliana, maisha yao ya mwisho hupenda kuyamalizia kwenye ukanda wa kijani na bila shaka mkoa wa Kagera ukiwa ni chaguo bora zaidi. Senene huanza safari yao wakati wa giza huku pembe zao zikiwa zimeangalia chini na mara waonapo mapambazuko hujificha chini kwenye nyasi.

Pengine ndiyo sababu wafanya biashara wa senene hufanikiwa kuwahadaa kwa mwanga mkali wa taa,na mara kadhaa makundi makubwa ya senene huletwa na mawimbi ya maji baada ya mapambazuko kuwakuta kwenye maeneo ya ziwa Viktoria.

Senene hupatikana mahali pengi duniani ingawa hutofautiana kutokana na mazingira na ikolojia ya eneo hilo.Madume hutoa mlio maalmu kuwavutia majike ingawa pia milio hiyo hutofautiana kutokana na aina ya senene na kundi lake.

Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Chakula na Kilimo duniani(FAO)ya mwaka 1999 katika utafiti wake wa ‘Non-wood Forest Product in Tanzania’umebainisha kuwepo kwa wadudu wengi wanaotumika kama kitoweo katika maeneo mbalimbali hapa nchini wakiwemo senene.

Utafiti huo pia unawataja wadudu kama kumbikumbi,swah,nywa na fihwa kuwa mbali na kutumika kama kitoweo pia huzalisha mazao mbalimbali ya chakula.
Hata hivyo senene na aina ya moja ya mchwa warukao wanatajwa kuwa na umuhimu mkubwa katika misitu ya miombo na kuwa wdudu wote hawa huuzwa katika masoko ya ndani baada ya wekewa chunvi na kukaangwa vizuri.

Katika miaka ya hivi karibuni safari ya senene kuelekea mashambani hufupishwa na wafanyabiashara ambao huwekeza pesa nyingi na kuwatega kwa kutumia taa zenye mwanga mkali.Katika eneo la Nyamkazi mjini Bukoba gharama ya kukodi eneo la kuweka mtego wa senene sio chini ya shilingi laki moja na waachuuzi wadogo humlipa ‘mwekezaji’shilingi elfu moja ili waruhusiwe kuokota senene watakaoanguka nje ya pipa lililofungwa taa.

Kwa vyovyote vile changamoto za mabadiliko ya tabia nchi na ushindani wa kibiashara utakifanya kitoweo cha senene ambacho ni sehemu ya utamaduni wa Wahaya uanze kusahaulika na pengine kubaki kwenye historia tu.

Senene kwa sasa imekuwa ikitumika kama kitega uchumi na hajira ya iana mbili. Kuna ajira ya kundi la Vijana wa Muda na Ajira ya kudumu kwa baadahi ya wajasiamari. Ajira ya muda ni kwa vijana hata ambao sio wahaya wamekuwa wajikiika katika kuwakamata na kuwauza wakati wa msimu tu na kundi la pili ununua senene nyingi amabazo uuzwa kidogo kidogo hadi msimu wa pili unapoanza.

Senene zimekuwa zikitumwa kwa njia ya bus, ndege kwa wahaya walioko ndani na nje ya Tanzania hadi huko famle za kiharabu, marekani, ulaya, austaria, Africa kusini na hata Brazil na kuogeza pato kwa wakazi wa Bukoba. Ukweli senene ni wadudu wanaongeza urafiki mkubwa kwani akitumiwa mtu kama zawadi anaweza kukuleta na kukujibu kwa zawadi kubwa mara dufu mfani senene za elfu tano ukimtumia rafiki mpendwa aliye ulaya anaweza kukutumia ngua kama suti yenye dhamaniya zaidi yalaki nane!!
Mazingira yatunzwe vizuri ili wanedlee kuleta neena mkoani kwetu
By William Oswald Rutta
Manager- Kiroyera Tours @2011

Tuesday, August 28, 2012

MKUTANO WA SIKU TATU WA LVRLAC WAANZA RASIMI LEO KWA WASHIRIKI WA MKUTANO HUO UPANDE WA TANZANIA WAKIPATIWA MAFUNZO YA UWEZESHWAJI YOTE HAYO YAKIFANYIKIA KATIKA UKUMBI WA MIKUTANO WA HOTELI MAARUFA MKOANI KAGERA YA YASILA..BLOG HII ITAZIDI KUKULETEA HABARI MBALIMBALI KUHUSIANA NA MKUTANO HUU KADRI YA MUDA UNAVYO KWENDA .


Mkurugenzi wa manispaa ya bukoba mkoani kagera bwana HAMISI KAPUTA ambaye ni mwenyeji wa mktano wa LVRAC akiwa katika pozi ya aina yake.




Wadau nao wamo.



kwanza kutambuana ilikuwa lazima.



Secritalieti katika kupokea wageni nayo ilikuwa vizuri.



Meza ya wakubwa wakijadili jambo.


Hawa ndio wadau kutoka unity trust of tanzania (UTT)  na Tanzania postal benk TPB ambao ndio wadhamini wa mkutano huu wa kimataifa wa LVRLAC hapa wakiwaza na kuwazua jinsi mkutano huo utakavyofana.





Baada ya kufahamina sasa wote ni wamoja hivyo tupige picha ya pamoja.




Meza ya watalii pia ilikuwa pembezoni hawa si wengine bali ni KILOYERA TOURS ambapo kushoti ni bwana WILLY KILOYERA mkurugenzi wa kampuni hiyo ya UTALII.


Kama ilivyo ada chai nayo ilikuwepo.